Waandishi
wa habari nchini wametakiwa kutojihusisha na maswala ya kisiasa katika utendaji
wao wa kazi ili kuandika habari za ukweli na usahihi.
Hayo
yamesemwa na Naibu Wziri JULIANA SHONZA
kwaniaba ya Waziri wa Habari,Tamaduni,sanaa Na Michezo katika maadhimisho ya
siku ya redio duniani ambayo kitaifa yamefanyikia Mjini DODOMA.
Naibu
waziri amesema waandishi wa habari wanajukumu la kufikisha habari kwa jamii ili
kulinda amani,na upendo kwa kujali utu wa mtu.
Amesema
vyombo habari vina nafasi kubwa katika jamii na kama vikitumika kwa mengo
sahihi itasaidia kuiunganisha jamii na serikali.
Maadhimisho
ya siku ya redio duniani kitaifa yamefanyika Mjini DODOMA huku yakibebwa na
kaulimbiu ya ‘redio na Michezo’ ambapo mgeni rasmi alikuwa ni Naibu waziri wa
Habari, Utamadunii sanaa na Michezo Mh JULIANA SONZA kwa niaba ya Waziri wa
Wizara hiyo Dr. HARRISON MWAKYEMBE.
No comments: