Header Ads

Jeshi la Polisi lawashukulia hatua kali madereva



Jeshi la Polisi Kitengo cha usalama Barabarani, Mkoani Mbeya limewafutia leseni Madereva watano wa Magari ya abiria baada ya kubainika wamekiuka sheria za usafirishaji.
 
Mkuu wa Polisi Kitengo Cha Usalama barabarani Mkoa wa Mbeya, Leopard Fungu
Akizungumza na Eatv Mkuu wa Polisi Kitengo Cha Usalama barabarani Mkoa wa Mbeya, Leopard Fungu amesema kume kuwepo na wimbi kubwa la ajali ambazo zimegharimu maisha ya watu wengi zinatokana na uzembe wa baadhi ya madereva kwa kutoheshimu sheria za usafirishaji.
"Katika kipindi hiki cha wiki tatu nimewafungia takribani madereva watano leseni zao. Tumechukua hivyo kutokana na hatutaki mchezo barabarani", amesema Leopard.
Kwa upande wake Afisa mfawidhi Sumatra kanda ya Mbeya, Denis Daudi amesema katika kudhibiti wimbi la ajali mkoani Mbeya, Mamlaka ya Usafiri wa Nchi kavu na majini Sumatra wameeleza kuwa katika oparasheni wanayoendelea nayo wamebaini makosa kadhaa kwenye magari na kuchukua hatua stahiki dhidi yao.
Kwa taarifa kamili mtazame hapa chini Mkuu wa polisi usalama barabarani mkoa wa Mbeya Leopard Fungu pamoja na Afisa mfawidhi Sumatra kanda ya Mbeya Denis Daudi

No comments:

Powered by Blogger.