Atakachofanya Lissu akirudi Tanzania chaanikwa
"Tundu Lissu tunataka akirudi asirudi ku-atend clinic, aje aingie kwenye mapambano moja kwa moja. Lissu ni kama kaka kwangu, alipopigwa risasi nilifadhaika sana, mpaka kesho nawaza hawa watu walikuwa na dhamira gani" Ole Sosopi.
Aidha Mwenyekiti huyo ameongeza kuwa "Lissu ni 'asset' kwa Tanzania na Mungu amemponya kutuonyesha, na ndio maana yupo mpaka leo".
Lissu ambaye ni Mbunge wa Singida Mashariki na Mwanasheria wa Chadema alipigwa risasi na watu wasiojulikana Septemba 7, 2017 alipokuwa kwenye maeneo ya nyumbani kwake Area D Jijini Dodoma wakati alipokuwa akirejea kutoka katika majukumu yake.

No comments: