Azam FC yakusudia kuipoteza Yanga mazima ?
Wakati
Azam FC imejipanga kupata matokeo mazuri katika mchezo wake huo ili
kuendelea kufukuzana na Yanga yenye alama 48 kuwania nafasi ya pili
kwenye msimamo, Majimaji yenyewe itakuwa ikijaribu kusaka pointi iweze
kujinusuru kushuka daraja msimu huu kwani hadi sasa ipo nafasi ya 13
ikiwa imejikusanyia jumla ya alama 24 ikiizidi pointi mbili Njombe Mji
inayoshika mkia.
Pamoja na hayo, tayari benchi la ufundi la Azam FC linalosimamiwa na Kocha Msaidizi Idd Cheche na Kocha wa timu ya Azam B, Meja Abdul Mingange, baada ya Kocha Mkuu Aristica Cioaba kwenda kusoma, limeshawaambia wachezaji wao juu ya umuhimu wa mechi zilizobakia katika kuhakikisha inashinda zote ili kujiweka pazuri kwenye msimamo.
Kwa upande mwingine, Azam FC itaendelea kuwakosa wachezaji wake mabeki Yakubu Mohammed, Swaleh Abdallah, Daniel Amoah, ambao ni majeruhi.
Wachezaji wengine walioukosa mchezo uliopita kutokana na kuwa wagonjwa, Nahodha Msaidizi Agrey Moris, kipa Razak Abalora, winga Enock Atta na kiungo Salum Abubakar ‘Sure Boy’, tayari wameanza mazoezi na wenzao kujiandaa na mchezo huo na litabakia ni jukumu la benchi la ufundi kuona kama wanafaa kucheza.
Pamoja na hayo, tayari benchi la ufundi la Azam FC linalosimamiwa na Kocha Msaidizi Idd Cheche na Kocha wa timu ya Azam B, Meja Abdul Mingange, baada ya Kocha Mkuu Aristica Cioaba kwenda kusoma, limeshawaambia wachezaji wao juu ya umuhimu wa mechi zilizobakia katika kuhakikisha inashinda zote ili kujiweka pazuri kwenye msimamo.
Kwa upande mwingine, Azam FC itaendelea kuwakosa wachezaji wake mabeki Yakubu Mohammed, Swaleh Abdallah, Daniel Amoah, ambao ni majeruhi.
Wachezaji wengine walioukosa mchezo uliopita kutokana na kuwa wagonjwa, Nahodha Msaidizi Agrey Moris, kipa Razak Abalora, winga Enock Atta na kiungo Salum Abubakar ‘Sure Boy’, tayari wameanza mazoezi na wenzao kujiandaa na mchezo huo na litabakia ni jukumu la benchi la ufundi kuona kama wanafaa kucheza.

No comments: