Header Ads

Kagame akiri kuteswa na viongozi wa Arsenal



Rais wa Rwanda Mh. Paul Kagame ameweka wazi kuwa kufanya vibaya kwa Arsenal ni tatizo la uongozi na sio kocha Arsene Wenger hivyo yeye kama shabiki wa timu hiyo ameumizwa na Wenger kuonbdoka bila taji.
Kagame ametumia mtandao wa 'Twitter' kuelezea mapenzi yake kwa klabu hiyo ambayo usiku wa kuamkia leo imeondolewa kwenye michuano ya Kombe la Europa.
''Kuhusu timu yangu ninayoipenda ya Arsenal, ni timu nzuri sana na imekuwa na kocha bora sana ambaye ni Wenger na hakupaswa kuwa na mwisho huu wa kuondoka bila kombe, lawama zote ziwaendee viongozi, lakini nitaendelea kuipenda Arsenal'' amendika Kagame.
Mapema mwezi April, Arsene Wenger alitamngaza kuondoka Arsenal mwishoni mwa msimu huu baada ya kuifundisha timu hiyo kwa miaka 22 huku akiipatia mafanikio kadhaa.

No comments:

Powered by Blogger.