Header Ads

RIPOTI MPYA YA KEMIKALI ZA SUMU:

RIPOTI MPYA YA KEMIKALI ZA SUMU: Korea Kaskazini imeingia katika sakata jingine la kudaiwa kupeleka vifaa mbalimbali nchini Syria ambayo vina uwezo wa kutengeneza silaha za kemikali, Taarifa ya Umoja wa Mataifa imesema.
Inadaiwa kuwa takribani meli 40 zimeshawahi kushusha vifaa hivyo kabla ya kuripoti kati ya mwaka 2012 na 2017, ripoti hiyo imebaini. Vifaa hivyo ambavyo vimejumuisha vigae vya kuzuia asidi, mabomba na valvu.
Ripoti hiyo ambayo bado haijatolewa imesema, wataalamu wa makombora wa Korea Kaskazini wamekuwa wakionekana katika vituo vya kutengenezea silaha vya nchini Syria.
Shutuma hizo zimekuja kufuatia ripoti mpya ya kutumika kwa kemikali ya klorini iliyotumiwa na vikosi vya Syria, ambayo serikali imekanusha madai hayo.


No comments:

Powered by Blogger.