Header Ads

Yanga yavunja mwiko Mtwara

Mabingwa watetezi wa ligi kuu soka Tanzania Bara Yanga SC, leo wamefanikiwa kuibuka na ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Ndanda FC kwenye uwanja wa Nangwanda Sijaona.

Ushindi huo umekuwa ni wa kwanza kwa Yanga ndani ya uwanja huo tangu timu ya Ndanda ipande kucheza ligi kuu soka Tanzania bara misimu mitatu iliyopita.
Mabao ya Yanga leo yemefungwa na kiungo Pius Buswita dakika ya 15 kipindi cha kwanza kabla ya Hassan Kessy kuongeza bao la pil;i dakika ya 29. Baadae Yanga ilipata penalti lakini kiungo Mkongo Papy Tshishimbi akampasia mlinda mlango wa Ndanda.
Bao la Ndanda FC limefungwa na Nassoro Kapama dakika ya 46 kipindi cha pili lakini halikusaidia timu hiyo kupata alama baada ya kushindwa kuongeza bao jingine hadi mpira unamalizika.
Yanga imetimiza mechi 19 za ligi msimu huu ikijikusanyia alama 40 na kuzidi kuzikimbia Azam FC yenye alama 35 na Singida United yenye alama 34 katika nafasi ya nne huku Simba wakiwa na alama 45 kileleni.

No comments:

Powered by Blogger.