Messi kurekebisha rekodi mbovu Italia ?
Pia Barcelona inakabiliwa na rekodi ya kutoshinda nyumbani kwa Roma ambapo katika mechi mbili walizokutana Roma imeshinda moja na kutoka sare moja. Roma waliifunga Barcelona mabao 3-0 mwaka 2002.
Katika mechi sita za mwisho ambazo Barcelona wamecheza nchini Italia hawajafanikiwa kushinda ambapo kati ya hizo wametoa sare nne na kufungwa mbili hivyo leo watakuwa na kazi ya kurekebisha rekodi hizo.

Kwa mujibu wa matokeo ya mechi ya kwanza iliyopigwa nchini Hispania wiki iliyopita ni kama Barcelona wameshaweka mguu mmoja nusu fainali, baada ya kufanikiwa kushinda mabao 4-1. Leo wanahitaji sare tu au wasifungwe kuanzia mabao 3-0.

No comments: