Watu 49 washikiliwa na Polisi Mtwara

Kamanda ameeleza kuwa mtandao wa wezi wa pikipiki ulikuwa na kambi katika kijiji cha Chikongo wilayani Tandahimba ambapo walikuwa wakiiba pikipiki na kwenda kuziuza kwa tajari mmoja ambaye huzisafirisha kuziuza nchini Msumbiji.
Katika tukio lingine Jeshi la Polisi Mtwara linawashikilia wanafunzi 9 wa Chuo Kikuu cha Stella Maris Mtwara na Daktari wa Hospitali ya Mission Nanyamba halmashauri ya mji wa Nanyamba kwa kosa la kutumia mitandao ya kijamii ikiwemo ‘Watsapp’ na Telegram’ kuhamasisha maandamano.

No comments: