Hascana amkataa Darassa
"Sihusiki kuongelea jambo lolote linalo muhusu Darassa kwasababu yeye ni 'brand' na mimi sio msemaji wa 'brand' ya Darassa bali mimi ni rafiki tu. So kama yeye ni 'brand' inabidi ajitokeze mwenyewe na kujizungumzia yeye kama yeye. Haitakuwa sahihi Hancana kuzungumzia brand ya mtu mwingine", amesema Hancana.
Mbali na hilo, Hancana amempongeza Darassa kwa kuweza kuhimili miki ya vitu vyote ambavyo watu walikuwa wanampakazia hasa kuhusu kujihusisha na dawa za kulevya.
"Nadhani hizi skendo huja kumpanikisha mtu ili wapate kumsikia anasemaje, 'sometimes' hivyo vitu vipo. Ninachomshukuru Darassa au kumpongeza ni amekuwa 'very strong' amesimama kwenye mipango yake anayoiamini 'no matter what', watu wanampanikisha kwamba anatumia dawa za kulevya mara amepotezwa kwenye muziki", amesisitiza Hancana.

No comments: