Header Ads

"Mfahamu majira yamebadilika" - Makonda



Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda amewataka wakandarasi waliopewa kazi ya kukarabati barabara za Jiji hilo kufanya kazi kwa umakini mkubwa ili waweze kuwatendea haki wananchi wanaolipa kodi pamoja na kuwapa onyo kuwa yeye hajawahi kuwa muoga katika kusimamia haki.
Makonda ametoa kauli hiyo leo Mei 09, 2018 wakati aliposhuhudia utiaji saini wa mikataba ya matengenezo ya barabara TARURA mkoani Dar es Salaam ambapo inajumuisha jumla ya Makampuni manane ambayo yatakuwa na kazi ya kukarabati barabara hizo.
"Nitoe rai kwa wakandarasi, sijawahi kuwa muoga wa kusimamia haki ya wananchi hasa walipa kodi, tunawapa dhamana hii ya kutujengea barabara kwa pesa zetu tena walipa kodi wanaonunua chumvi, mafuta ya taa, mchele wanakatwa. Ile asilimia wanayokatwa ndio inawapa nyie nafasi ya kupata ajira na  kazi ya kutujengea barabara. Fanyeni kwa kuwaheshimu wananchi hawa kwa uadilifu mkubwa mtengeneze barabara nzuri",amesema Makonda.
Pamoja na hayo, Makonda ameendelea kwa kusema "ule ujanja wenu ambao mliokuwa mnaufanya mfahamu majira yamebadilika kwa hiyo niwaombe pamoja na usimamizi utakaokuwepo wa TARURA lakini na nyinyi lindeni heshima ya makampuni yenu".
Kwa upande mwingine, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda amesema endapo watatengeneza barabara kwa kiwango kizuri basi wataendelea kupata kazi.

No comments:

Powered by Blogger.