Mugabe alitosa bunge
Kwa
mujibu wa vyombo vya habari nchini Zimbabwe Mugabe alitakiwa kwa mara
ya kwanza kutokea mbele ya kamati Mei 23 , 2018 saa 3 asubuhi na
kutotokea kwake kulidhaniwa kuwa ni sababu ya uzee hivyo alishindwa
kufika muda wa asubuhi.
Kwa mara ya pili Mugabe alitakiwa kufika tarehe 28 Mei 2018 saa 7 mchana lakini pia ameshindwa kufika hivyo kama sheria inavyosema ataitwa mara ya 3 kabla vyombo vya dola havijapewa kazi ya kumfikisha Bungeni kwa nguvu.
"Tuliandika barua kwa Rais mstaafu kwa mara ya pili kuja lakini ameshindwa na tutaandika kwa mara ya mwisho kama inavyotakiwa na sheria, "Mbunge wa Themba Mliswa alisema.
Rais huyo mwenye umri wa miaka 94 aliyeongoza kwa muda mrefu hadi alipotolewa madarakani Novemba 2017, ametakiwa kufika Bungeni hapo Juni 11, 2018 bila kukosa.
Kwa mara ya pili Mugabe alitakiwa kufika tarehe 28 Mei 2018 saa 7 mchana lakini pia ameshindwa kufika hivyo kama sheria inavyosema ataitwa mara ya 3 kabla vyombo vya dola havijapewa kazi ya kumfikisha Bungeni kwa nguvu.
"Tuliandika barua kwa Rais mstaafu kwa mara ya pili kuja lakini ameshindwa na tutaandika kwa mara ya mwisho kama inavyotakiwa na sheria, "Mbunge wa Themba Mliswa alisema.
Rais huyo mwenye umri wa miaka 94 aliyeongoza kwa muda mrefu hadi alipotolewa madarakani Novemba 2017, ametakiwa kufika Bungeni hapo Juni 11, 2018 bila kukosa.

No comments: