Nimesikitishwa sana - Wenger
“Najisikia vibaya kuicha timu ikiwa katika hali ya kutolewa katika mashindano kama hivi, itanichukua muda kusahau, nitaangalia cha kufanya hapo badae ila kwasasa bado sijaamua kitu chochote” amesema Wenger.
Wenger ameongeza kuwa timu ya Arsenal bado ina wachezaji wazuri ambao wataweza kutoa ushindani kwa miaka ya mbeleni na kuutaka uongozi wa timu hiyo kupanga mipango bora ya kujiandaa na msimu ujao.
Timu ya Arsenal iliondoshwa katika mashindano ya Europa baada ya kufungwa goli 1-0 na Atletico Madrid katika mchezo wa nusu fainali na kuhitimisha msimu wa mwisho kwa kocha wao Arsene Wenger ambae ataiacha klabu hiyo msimu huu baada ya kuifundisha kwa miaka 22.

No comments: