TAMKO LA MUHESHIMIWA WAZIRI WA HABARI UTALII NA MAMBO YA KALE KATIKA UHURU WA VYOMBO VYA HABARI DUNIANI MEI 3 2018
Ulimwengu unaadhimisha siku ya uhuru wa vyombo vya habari
duniani.Maadhimisho hayo yanafanyika kesho jijini Accra Ghana
yakiongozwa na shirika la elimu sayansi na utamaduni la umoja wa mataifa
UNESCO
Ni siku ambayo dunia inatathmini hali ya uhuru wa vyombo
vya habari duniani kote ambapo inatolewa michango ya kutetea vyombo vya
habari vinavyokabiliana na mashambulizi pamoja na kuwakumbuka waandishi
wa habari waliopoteza maisha yao wakiwa kazini.
Kila mwaka zaidi ya waandishi maadhimisho 100 ya kitaifa
yanafanyika kuiadhimisha siku hii na shirika la elimu sayansi na
utamaduni la umoja wa mataifa UNESCO ndilo linaloongoza maadhimisho hayo
katika kila pembe ya dunia.
Kauli mbiu ya mwaka huu ni ‘wajibu wa Uongozi Vyombo vya habari,haki na utawala wa sheria.
Kauli mbiu ya mwaka huu ni ‘wajibu wa Uongozi Vyombo vya habari,haki na utawala wa sheria.
Ndugu wananchi serikali ya mapinduzi Zanzibar inatambuwa
umuhimu wa siku hii ambayo ilitangazwa na baraza kuu la umoja wa mataifa
mwaka 1993 kufuatia pendekezo la mkutano mkuu wa 26 wa UNESCO mwaka
1991 lililotokana na azimio la windhock la waandishi wa habari wa afrika
la mwaka huo huo kuhusu maadhimisho ya uhuru wa vyombo vya habari
Ndugu wananchi azimio hilo vile vile liliridhia kuanzishwa
kwa taasisi ya vyombo vya habari kusini mwa afrika MISA Ambayo wote
tunajuwa mchango wake katika kupigania uhuru wa vyombo vya habari
maadili na weledi katika tasnia ya uandishi wa habari.
Siku ya uhuru wa vyombo vya habari mwaka huu inaonesha
uhusiano kati ya serikali kwa upande mmoja na uhuru wa vyombo vya habari
haki na utawala wa sheria.
Ndugu wananchi sekta ya ahbari ni sekta za huduma za
jamiihapa nchini. Sekta hii inatowa huduma ambayo ni haki ya msingi ya
raia kama inavyotamkwa kwenye katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984. Ibara ya
18 ya katiba inasema
1. Kila mtu yuko huru kuwa na maoni yoyote na kutoa nje
mawazo yake na kutafuta kupokea na kutoa habari na dhana zozotekupitia
chombo chochote bila ya kujali mipaka ya nchi na pia ana uhuru wa
mawasiliano yakekutoingilia kati.
2. Kila raia ana haki ya kupewa taarifa wakakti wowote
kuhusu matukio nchinina duniani kote ambayo ni muhimu kwa maisha ya na
shughuli za wananchi na pia ni juu ya masuala muhimu kwa jamii. Aidha
kutoa na kupokea habari kunatambuliwa duniano kote kuwa ni moja ya haki
za binaadamu.
Ndugu wananchi umoja wa mataifa na umoja wa afrika zina
matamko rasmi ambayo serikali imeridhia kuhusu haki ya kupokea na kutoa
habari.
Haki hii,kama zilivyo haki nyengine zote hutolewa kwa kuzingatia wajibu wa kila raia kwa jamii na uhuru binafsi wa binaadamu.
Ndugu wananchi,serikali ya mapinduzi Zanzibar itaendelea kuheshimu na kukuza uhuru wa vyombo vya habari na uhuru wa kujielezea kama ilivyoelekeza katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984.
Haki hii,kama zilivyo haki nyengine zote hutolewa kwa kuzingatia wajibu wa kila raia kwa jamii na uhuru binafsi wa binaadamu.
Ndugu wananchi,serikali ya mapinduzi Zanzibar itaendelea kuheshimu na kukuza uhuru wa vyombo vya habari na uhuru wa kujielezea kama ilivyoelekeza katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984.
Ndugu wananchi kuna mafanikio chanya kwa upande wa vyanzo
vya habari hapa Zanzibar hali ilivyo leo tofauti sana na ilivyokuwa huko
nyuma, serikali imekuwa ikihimiza maafisa wakuu kutoa ushirikiano kwa
vyombo vya habari.
Ndugu wananchi mara kadhaa tumemsikia Rais wa Zanzibar na
mwenyekiti wa baraza la mapinduzi, mheshimiwa Dk,Ali Mohd Sheni
akihimiza viongozi wenzake serikalini kushirikiana kwa karibu na
waandishi wa habari.
Ndugu wananchi, Ripoti mbali mbali zile za waandishi
wasiokuwa na mipaka {Repoters Without Borders}, vyama vya kutetea
waandishi wa habari vinasema kwamba uhuru na usalama wa waandishi wa
habari umeonekana kuwa mdogo na usiowapa uhakika wa kufanya kazi zao kwa
ufanisi katika mataifa kadhaa.
Ndugu wananchi, hali hiyo ni tofauti sana na hapa Zanzibar
ambapo ukisoma katika magazeti ukisikiliza redio ukitazama televisheni
majarida mitandao ya kijamii serikali imekuwa ikikosolewa wazi wazi.
Wakati mwengine waandishi wamevuka mipaka kwa kuinanga
serikali, lakini hakuna aliyechukuliwa hatua za kisheria au kutishwa,
sisemi sasa Serikali ifanye kinyume chake la hasha lakini naonesha jinsi
gani serikali ilivyo na uvumilivu kwa kujenga jamii yenye kuvumiliana
kimawazo.
Ndugu wananchi, wakati huu tukiadhimisha siku ya uhuru wa
vyombo vya habari sina budi kumshukuru kwa dhati rais wa Zanzibar na
mwenyekiti wa baraza la mapinduzi Mheshimiwa Dk Ali Mohd Sheni kwa
uamuzi wake wa kuviimarisha vyombo vya habari vya serikali.
Mageuzi makubwa katika kulijengea uwezo Shirika La
Utangazaji Zanzibar mikutano yake na waandishi wa habari pamoja na
uwazi,kusimamia misingi ya utawala bora ushirikishwaji wa vyombo vya
habarikatika shuhuli mbalimbali za serikali na mengineyo ni thamira
tosha ya serikali katika kukuza uhuru wa vyombo vya habari.
Ndugu waandishi wa habari nimalizie kwa kusema kuwa suala
moja ni muhimu katika hayo yote ni jukumu la uandishi wa habari
unaozingatia ueledi, uzalendo heshima kwa jamii na umuhimu wa kuwalinda
wale ambao wanahusika katika taaluma hii inayohudmia umma.
Asanteni.
Asanteni.




No comments: