Header Ads

"Ukishindwa kuleta manufaa tutakurudisha" - JPM




Rais Dkt. John Magufuli amesema amesikitishwa na vitendo vya Mabalozi kushindwa kutekeleza maagizo yake aliyowapa ya kumpa taarifa juu ya utendaji kazi wao na manufaa ambayo Tanzania imeyapata kwa uwepo wa kila Balozi katika nchi aliyopangiwa kila robo mwaka.
Dkt. Magufuli ametoa kauli hiyo leo Mei 10, 2018 wakati alipokuwa anazungumza mara baada ya kumaliza kumuapisha Mhe. Alphayo Japani Kidata kuwa Balozi wa Tanzania nchini Canada na Bw. Msalika Robert Makungu kuwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Tabora, Ikulu Jijini Dar es Salaam na kuwataka viongozi hao kwenda kuchapa kazi kwa juhudi na maarifa na kwa manufaa ya Taifa na sio kufanya mambo ndivyo sivyo.
"Nataka nijue katika kipindi ambacho Mhe. Balozi ameteuliwa kuiwakilisha Tanzania katika nchi fulani, nchi imenufaikaje na uwepo wake kwenye nchi ile?. Kuteuliwa sawa lakini sio lazima ukae katika ubalozi huo kwa kipindi chote ulichopangiwa, ukishindwa kuleta manufaa unarudishwa na huko anapangiwa mtu mwingine atayeleta manufaa kwa nchi", amesema Rais Magufuli.
Kwa upande mwingine, Rais Magufuli ameipongeza Wizara ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) kwa kufanya kazi nzuri katika sekta ya Elimu na Afya

No comments:

Powered by Blogger.