Singida yagoma kufungwa na Yanga
Yanga ilibidi wasubiri dakika za mwisho kipindi cha kwanza ndipo wakasawazisha bao kupitia kwa mlinzi wake wa kati Abdallah Shaibu maarufu kama Ninja baada ya kumalizia kwa kichwa kona iliyopigwa na Ibrahim Ajib.
Matokeo hayo sasa yanaifanya Yanga kufikisha alama 47 kwenye michezo 22 ikiwa nyuma kwa alama 5 mbele ya vinara wa ligi Simba SC wenye alama 52 katika mechi 22. Singida United imefikisha alama 37 ikiendelea kusalia katika nafasi ya tano baada ya michezo 23.

Kesho vinara wa ligi hiyo Simba SC watashuka kwenye uwanja wa taifa kuwakaribisha Mbeya City kwenye mchezo wao wa raundi ya 23 huku Azam FC wakiwa ugenini kucheza na Ruvu Shooting kwenye uwanja wa Mabatini Mlandizi.

No comments: